Psalms 35:1-6
Kuomba Msaada: Kuokolewa Kutokana Na Maadui
(Zaburi Ya Daudi)
1 aEe Bwana, pingana na wale wanaopingana nami,
upigane na hao wanaopigana nami.
2 bChukua ngao na kigao.
Inuka unisaidie.
3 Inua mkuki wako na fumo ▼
▼ Fumo ni sawa na sagai, maana yake ni mkuki mfupi.
lakodhidi ya hao wanaonifuatia.
Iambie nafsi yangu,
“Mimi ni wokovu wako.”
4 dWafedheheshwe na waaibishwe
wale wanaotafuta uhai wangu.
Wanaofanya shauri kuniangamiza
warudishwe nyuma kwa hofu.
5 eWawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,
malaika wa Bwana akiwafukuza.
6 Njia yao na iwe giza na ya utelezi,
malaika wa Bwana akiwafuatilia.
Copyright information for
SwhKC